Media Centre
Speech

Honourable Prime Minister Kassim Majaliwa, Prime Minister of the United Republic of Tanzania, Honourable Jerry William Sila, Minister of Information Communication and Information Technology, Honourable Albert John Chalamila, Regional Commissioner of Dar es Salaam, Mr. Mohammed Kames Abdullah, Permanent Secretary of the Ministry of Information Communication and Information Technology, Dr. Nkundwe Moses Mwasaga, Director General of the ICT Commission, distinguished guests.
First of all, I’m honoured to stand before you on behalf of Huawei Tanzania to deliver these remarks. I would like to thank the organisers for the invitation and the opportunity to be here among so many distinguished guests and leaders as we discuss the digitalization of this beautiful country.
Over the past few years, we have witnessed huge progress in Tanzania’s journey towards digitalization. On behalf of Huawei Tanzania, I would like to commend the Government of Tanzania and the leadership of Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan for her vision of fostering innovation, inclusion, and sustainable development through digital technologies.
For over 15 years, Huawei has been privileged to be a partner in Tanzania’s digital transformation journey. Our contribution spans across various sectors, which have brought connectivity to millions of Tanzanians and bridged gaps, not only in cities but also in the most remote corners of this beautiful country.
Among many areas we can mention:
● We helped to upgrade Tanzania’s network from 2G to 3G, 4G, and even 5G.
● We helped to construct the National ICT Backbone, connecting all 26 regions and neighbouring countries.
● We provided high-speed network coverage on Mount Kilimanjaro together with TTCL.
● And most importantly, we launched the DigiTruck Program in collaboration with our partners. In February this year, we had the honour to present this program to the Honourable Prime Minister.
Today, the DigiTruck is already launched and operational, covering regions of Tanzania. More regions will be covered in the coming several years.
Additionally, Huawei has established 19 ICT Academies with universities and institutes, training over 6,000 students in ICT skills.
Honourable Prime Minister, as we look to the future, Huawei is determined to continue our work in supporting Tanzania’s digital transformation agenda. In light of that, please allow me to reflect on the powerful message you delivered at the recent United Nations General Assembly. You spoke about the need for urgent clean energy solutions, stressing that sustainable energy is not only essential for the environment but also for the development of our communities.
This call to action aligns well with Huawei’s mission: We believe that the rule of creativity must be paired with reliable and clean energy sources. In response to that, Huawei is excited to announce our Smart Village Initiative with the Rural Solar Power Microgrid Solution. This initiative aims to bring sustainable energy to the rural villages without power grid access. It will enable schools, clinics, and homes to stay connected and powered, creating digital livelihoods. This is where ICT and energy intersect to build sustainable power, connectivity, and digital services, ensuring that no one is left behind.
Honourable Prime Minister, to sum up, I would like to thank the Ministry of ICT and the ICT Commission for their outstanding cooperation in taking our common visions forward. Moreover Huawei is committed to the concept of 'In Tanzania, and For Tanzania' and will continue contributing to the development of Tanzania’s digital economy, ensuring that no one is left behind. As the famous African saying goes, ‘If you want to go fast, go alone. If you want to go far, go together.’ So together, let’s digitalize Tanzania, heading to a bright future.

Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jerry Slaa, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Viongozi wote mlio Meza Kuu, na washiriki wa kongamano kwa ujumla.
Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa niaba ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Kamati ya Bunge ya Miundombinu, tunayo furaha kubwa sana kuungana na wewe leo hii kushuhudia kongamano hili la TEHAMA, linalofikia tamati. Mheshimiwa Waziri Mkuu, sisi kama Bunge ni mashahidi wa shughuli za Serikali ambazo Kamati ya Bunge ilipitisha bajeti yake. Tunaipongeza sana Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa na jitihada za kipekee katika kufanya mapinduzi makubwa ndani ya sekta hii ya wizara ya TEHAMA.
Kuna mabadiliko makubwa sana ambayo yamefanywa na Serikali. Wizara hii hapo awali ilikuwa ikipokea fedha kidogo, lakini kwa dhamira thabiti ya Mheshimiwa Rais, kwa kipindi cha miaka mitatu (3) iliyopita, wizara hii imeongezewa fedha nyingi, na kuifanya kuwa moja ya wizara zilizovunja rekodi kwa kupata fedha nyingi. Matokeo ya uwekezaji huu yameanza kuonekana.
Taasisi nyingi zilizo chini ya Wizara ya TEHAMA zimepata mabadiliko makubwa, na tumeshuhudia karibu kila taasisi ikiwa na uwekezaji mkubwa kutoka Serikalini. Kwa upande wa Mkongo wa Taifa, mmefanya kazi nzuri sana. Tumepanga na kuongeza fedha ambazo zimeleta matokeo chanya, karibu kila kona tumeona upatikanaji wa huduma za mkongo huu, ambao sasa unafika hadi kwenye maeneo ya wilaya.
Ukitaka kufahamu umuhimu wa sekta hii, hitilafu ndogo kwenye mkongo wa Taifa husababisha madhara makubwa nchi nzima. Lakini tumeona jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita, kuhakikisha Posto Kodi zinafikishwa kwenye maeneo karibu kila sehemu. Ukienda vijijini, unashuhudia mabadiliko makubwa yaliyofanywa na Serikali. Mheshimiwa Waziri Mkuu, tuna sekta ya Mawasiliano kupitia TCRA, kuna uwekezaji mkubwa ambao sisi kama Bunge tumeona, na kuna mengi mengine yanayofanywa na Serikali. Bila juhudi hizi kubwa, tungekuwa na wakati mgumu sana!
Mheshimiwa Waziri Mkuu, namshukuru sana Waziri mwenye dhamana, kwa kazi kubwa ambayo anasimamia kwenye wizara hii. Anajitahidi sana katika utendaji wake, na leo hii, tunapozungumza, Mheshimiwa Waziri, kwenye kamati tuna mswada ambao upo Bungeni, na yeye anausimamia na kuusukuma ili uweze kusaidia taasisi zilizo chini ya wizara yake.
Tunaishukuru sana Serikali, na sisi kama Bunge, tunaahidi kuiunga mkono Serikali kwa sababu tunaona maendeleo makubwa yaliyofanywa na Serikali pamoja na dhamira yake. Wizara hii, ingawa wengine wanaweza kuiona kama wizara ndogo, imebeba karibu kila kitu ambacho Serikali inakitegemea. Tunakushukuru sana, Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa kushiriki nasi.
Asante sana!

Mheshimiwa Waziri Mkuu, Viongozi wa Meza Kuu, Washiriki wa Kongamano, Mabibi na Mabwana. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kazi Iendelee!
Mheshimiwa Mgeni Rasmi, kwanza napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutupa afya njema na kutuwezesha kushiriki kilele cha Kongamano la Nane la Mwaka wa Tehama. Pia ningependa kutoa shukrani za dhati kwako, Waziri Mkuu, kwa kukubali kuwa Mgeni Rasmi kwenye kilele cha kongamano hili. Tunakushukuru sana!
Mheshimiwa Mgeni Rasmi, tulikuwa tumeandaa hotuba fupi ya kukukaribisha, lakini niseme kwa dhati, umekuja mapema na mengi tuliyopanga kuyasema umeyaona tayari kwenye mabanda. Wazungumzaji waliotangulia wamesema mengi, na vile vile tuliwasilisha presentation kwa njia ya video iliyozungumzia mafanikio makubwa ya kisekta ndani ya Wizara ninayoisimamia. Ukianzia na upatikanaji wa mtandao wa simu nchini, tumefikia asilimia 89 kwa mtandao wa 3G na asilimia 84 kwa mtandao wa 4G. Mtandao wa mkongo wa taifa umeenea hadi kilomita 13,820, na mtandao wa makampuni ya simu kupitia mfumo wa Corsoteum umejengwa kwa kilomita 1,592.
Mheshimiwa Mgeni Rasmi, kituo chetu cha mawasiliano na uhifadhi wa data, NIDC, tayari kimehamishiwa TTCL. Pia napenda kukuarifu kuwa Wizara imeanza maandalizi ya urushaji wa satellite, na mkakati wa miaka mitano kwa programu za anga za juu umeanza kuandaliwa. Haya maandalizi yanahusisha utungwaji wa sera, sheria, na mikataba ya kimataifa kuhusiana na masuala ya anga za juu.
Kwa upande wa miradi, Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) imepata mradi wa utafiti wa kuwezesha urushaji wa satellite kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa kupitia taasisi ya United Nations Office for Outer Space Affairs (UNOSA) pamoja na Taasisi ya Anga za Juu ya Japan (JACSA).
Mheshimiwa Mgeni Rasmi, umeona pia kwenye banda la Wizara mfumo wa Anwani za Makazi (NAPA) na faida zake kwa taifa letu. Vilevile, umejionea jinsi Wizara inavyotekeleza maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuhakikisha mifumo inasomana, kama vile Jamii Number, Jamii Malipo, na Jamii Exchange.
Kongamano hili la nane limefanyika chini ya kaulimbiu isemayo: “Kutumia Uwezo wa Akili Bandia na Robotics kwa Ajili ya Mapinduzi ya Kiuchumi na Kijamii.” Kama ulivyopokea taarifa, kongamano limefanyika kuanzia Jumapili, na leo tumekualika kulifunga. Kaulimbiu hii inaweka msingi wa matumizi ya teknolojia zinazoibukia, kama vile akili bandia, robotics, na uchambuzi wa Big Data, katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.
Mheshimiwa Mgeni Rasmi, leo hii utatoa tuzo kwa washindi wa mashindano ya vijana wa Afrika kuhusu Robotics na Akili Bandia (Artificial Intelligence and Robotics Competition). Pia, utatoa tuzo kwa vijana wa Kitanzania waliopata mafanikio kwenye mashindano ya kimataifa kuhusu teknolojia hizi. Hii ni fursa kubwa kwa taifa letu, kwani mashindano haya yanafanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika, na Tanzania imechaguliwa kuwa mwenyeji wa kilele cha mashindano haya, yaliyoratibiwa na Taasisi ya Maendeleo ya Afrika (AUDA–NEPAD).
Mheshimiwa Mgeni Rasmi, Serikali imeanza ujenzi wa Chuo cha Teknolojia ya Kidigitali (Digital Technology Institute) kule Nala, Dodoma, ambacho kitakuwa kituo cha mafunzo ya vitendo kwenye teknolojia zinazoibukia.
Mheshimiwa Mgeni Rasmi, kazi yangu kubwa ni kukuomba masuala yafuatayo:
● Tunakuomba upokee zawadi ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutoka AUDA–NEPAD.
● Tunakuomba upokee zawadi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, ambayo ni mfano wa chuo kitakachojengwa Nala, Dodoma. Tunakuomba utuombee kwa Mheshimiwa Rais ili chuo hiki kiitwe Dr. Samia Suluhu Hassan Digital Technology Institute.
● Tunakuomba upokee zawadi yako kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, ambayo ni mfano wa satellite, ikiwa ni ishara ya mwanzo wa safari ya utekelezaji wa programu ya miaka mitano ya masuala ya anga za juu, ijulikanayo kama "From Mount Kilimanjaro, the Peak of Africa, to Space."
● Tunakuomba utoe tuzo, vyeti, na zawadi kwa washindi.
● Mwisho, tunakuomba ulihutubie hadhara hii iliyokusanyika mbele yako.
Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa heshima na taadhima, sasa nakukaribisha kuanza na shughuli hizo niliyotangulia kuyataja, na baada ya hapo uzungumze na hadhara iliyoko hapa. Mheshimiwa Waziri Mkuu, karibu sana!
Mshereheshaji kisha alimkaribisha Waziri Mkuu kwa ajili ya kuanza shughuli za utoaji wa zawadi, akianza na zawadi ya kwanza mpaka zawadi kwa Waziri Mkuu.
Baada ya hapo, Mshereheshaji (M.C) alimkaribisha Dada Yvonne kutoa maelezo mafupi kabla ya kuanza kwa shughuli za utoaji zawadi.

Honourable Prime Minister, Kassim Majaliwa Majaliwa(MP), Her Excellency Dr. Madam Nardos Bekele Thomas, Hon. Minister Jerry Slaa (MP), Permanent Secretary of the Ministry of ICT, Mr. Muhammad Abdullah, our esteemed diamond sponsor for the inaugural of the African Youth in Artificial Intelligence and Robotics Competition, BADEA; our other partners including SADC, the climate robotics network, WeRobotics, the flying labs network and all invited guests, ladies and gentlemen, all protocols observed.
In the interest of time, I would like for the concept of inaugural of the African Youth in AI and Robotics to be streamed.